Siasa
 

BARUA KUTOKA DAR ES SALAAM ISLAMIC CLUB

Mheshimiwa Balozi wa Denmark
Nchini Tanzania
Dar es Salaam

Mheshimiwa,

Barua hii inawasilisha malalamiko kwa serikali yako kutoka kwa SHURA juu ya machapisho ya vikatuni vinavyomuonyesha Mtukufu Mtume, (Rehema na amani iwe juu yake) kwenye gazeti la Denmark, Jyllads - Posten.

SHURA inawakilisha madhehebu zote za Kiislamu nchini Tanzania, na Dar-es-Salaam Islamic Club ndio sekretariati yake.

Machapisho hayo sio yenye kukufuru tu katika Uislamu bali pia ni ya kichokozi yenye kuchukiza sana kwa sababu Mtume pia alionyeshwa kama mtu wa vurugu.

Serikali yako kwa upande wake imeonyesha masikitiko yake tu lakini labda ikiwa upande mmoja na gazeti hilo kwa ngao ya Uhuru wa Kuongea, ingawa gazeti lenyewe kwa
upande wake limeomba radhi.

Mheshimiwa, kila uhuru unayo mipaka uliozuiliwa kwayo unaoamriwa kibusara na murua wa msingi, maadili na dhana iliyozoeleka ya uwajibikaji kiasi kwamba wakati jamii inapofaidika kwa uhuru huo, vile vile inakuwa haidhofishwi kuhusiana na umoja na
utangamano utokanao nao.

Pale uhuru unapodhalilishwa kama utamaduni katika nchi, serikali yake inatakiwa kuuchunga kwa kutunga sheria. Kushindwa kwa serikali yoyote kufanya hivyo inatwaawajibu unaolingana kwa matokeo ya kashfa hiyo.

Utakubali bwana kwamba watu wenye namna mbalimbali za Imani wanalazimika kutetea maadili tofauti. Kwa suala la wafuasi wa Uislamu, maadili yao yanahusika kwenye Uislamu wenyewe, hususan pale ambapo Uislamu pia ni mfumo wa maisha juu yao.

Kwa hiyo, kutegemea maadili ya kawaida ya walio wengi, hasa kama wengi wao ni wa namna ya kilimwengu, kuyabadilisha na maadili ya kidini ya walio wachache, ni sawa na kunyimwa uhuru wa kuabudu.

Kinachokera sana Mheshimiwa ni ule utambuzi- kama ni sahihi au wa makosa- kwamba machapisho hayo yalitiwa hamasa na chuki dhidi ya Uislamu. Na kwa kweli, wakati huyo mhariri wa gazeti hilo bila kutegemea, alipoulizwa katika kipindi cha HARDTALK cha BBC kilichofanyika Copenhagen siku ya Ijumaa kwamba itakuwa ni sawa sawa kwake kwa hiyo, kuchapisha katuni ya Rabbi yenye nembo ya Nazi, kama ingeamuliwa hivyo chini ya ngao ya uhuru wa kuongea, alionekana kulikwepa swali hilo.

Tunaona mheshimiwa, kwamba Serikali za magharibi zina wepesi sana wa kuwahakikishia wayahudi, na kwa kweli hivyo ndivyo ilivyo, katika kuonekana kwa kipinga Usemiti kidogo sana kwenye nchi zao. Panatokea hata hivyo kukosekana kwa mazingatio kama hayo kwa Waislamu pale wanapokosewa ambao ni wa kukusudiwa zaidi kuliko kukosewa.

Mheshimiwa ipo haja ya kutangamanisha hali ya kuishi pamoja kwa amani katika jamii ya wanadamu kwa kiwango cha ulimwengu hasa ambapo nchi yako kama nyinginezo huko
magharibi hapo zinafaidika vya kutosha, pamoja na mambo mengine, kutokana na biashara ya nje. Kufanikiwa zaidi juu ya soko la wengine na kuonyesha heshima inayostahili juu ya hisia zao za kidini lazima viende pamoja mkono kwa mkono. Hakuna gazeti au chombo chochote cha habari kinachoweza kuachiwa kuvuruga uwiano huu nyeti na mazingatio ya kulipiza.

Mheshimiwa, tumejenga hoja njema kwa serikali yako kufanya zaidi kuliko maelezo ya juu ya masikitiko kama itachagua kukubali ukubwa wa kosa lililotendeka chini ya milki ya utawala katika nchi yako.

Kwa wakati huu tunaishia hapa.

Wako mwaminifu

Balozi Abbas K. Sykes
Mwenyekiti
Dar-es-Salaam Islamic Club
S.L.P. 3125.

~Juu

 

   
   Vitabu vya Kiarabu
» Orodha ya bei ya Vitabu vya Kiarabu
 
 
  Copyright © Alitrah, 2003. All rights reserved