|
ULIMWENGU
WA SHIA UNAOMBOLEZA JUU YA MASHAMBULIZI
YA KWENYE HARAM TUKUFU
Madhehebu ya Shia duniani
kote, ynaomboleza kwa huzuni kubwa na hisia,
mashambulizi
ya kupigwa mabomu kwenye Haram Tukufu iliyoko
Samarrah (Kaskazini ya Baghdad ndani
ya Iraqi) ya Wajukuu na kizazi cha moja
kwa moja cha Nyumba ya Mtukufu Mtume
Muhammad (s.a.w.) yaani, Imam Ali Naqi "al-Hadi",
na Imam Hassan "al-Askari" (amani
iwe juu yao wote). Haram hizi Tukufu, zinahifadhi
Misikiti ambamo Waislamu huitwa
kwa ajili ya Swala, mara tano kwa siku,
kila siku.
Haifikiriki kwa Muislam
yohyote kuvuruga kwa namna yoyote (achilia
mbali shambulio
la mabomu) sehemu takatifu yenye taadhima
kama hiyo ambapo Waislam hukusanyika kwa
ajili ya Ibada ya Mwenyezi Mungu Mtukufu,
Muumba wa Ulimwengu.
Haram hii ya Samarrah inayohifadhi
Kuba ya wawili kati ya hawa watu mashuhuri
katika
historia ya Uislamu pia ni sehemu yenye
umuhimu mkubwa wa kihistoria. Kwani, ndani
ya eneo la Haram Tukufu hiyo, ni sehemu
ya "ghaiba" (aliyochukuliwa na
Allah,
kuwekwa mfichoni mwaka 260 Hijiria) ya Imam
Mahdi, mtoto wa Imam Hasan al-Askari.
AL-MAHDI (kwa mujibu wa itikadi ya kiislamu)
atajitokeza hapo baadae kuujaza
ulimwengu na haki kwani utakuwa umejaa ukandamizaji
na dhulma.
Jumuiya ya Shia ya Tanzania
inalaani vitendo vya kiwoga vya namna hiyo,
vilivyochochewa kutokana na tamaa ya madaraka
kutoka kwa mtu yeyote, au kundi lolote
au mataifa yoyote.
Kwa ajili ya kuomboleza,
Jumuiya ya Shia ya Tanzania imeitisha kipindi
cha siku 7 za
maombolezo kuanzia tarehe 23 Feb. 2006.
Jumuiya ya Khoja
Shia Ithnaashari Jamat ya Dar-es-Salaam
|